Kwa habari zaidi kuhusu ORBIT tembelea tovuti ya: www.orbit-tz.com
KWA MAONI AU USHAURI TUTUMIE KWENYE E-mail: kusinileo@gmail.com

Sunday, 13 April 2014

Maalim Ngurumo afariki dunia leo



Ngurumo akiwa na Asha Baraka wakati wa Uhai wake


 Na Mwandish wetu
MWANAMZIKI  Mkongwe nchini Maalimu Ngurumo amefariki dunia leo Jijini  Dar es Salaam.
Ngurumo  amefariki wakati akiwa akipata matibabu ya ugonjwa katika hospitali ya Taifa Muhimbili.
 Akizungumza kwa njia ya simu Mpiga Gitaa na Kinanda wa bendi ya Msondo, Abuu Ridhwani (Toto) alisema taarifa za awali zinasema Mzee Ngurumo alipelekwa hospitali ya Muhimbili toka jana baada ya hali yake kuwa sio mzuri.
Taarifa zinasema kuwa msiba utakuwa Nyumbani kwake Tabata Geleji na mipango ya mazishi itafanya hadi pale familia itakapo kutana na mazishi ya kuwa nyumbani kwake Kisarawe katika kijiji cha Masaki.
Hadi tunaingia mtamboni timu nzima ya kusiniblog inaelekea Tabata na hivyo tutaelezana kila kitu kitakachoendelea
Inna Lillah Wainnah Illahi Raajiun .

No comments:

Post a Comment