Kwa habari zaidi kuhusu ORBIT tembelea tovuti ya: www.orbit-tz.com
KWA MAONI AU USHAURI TUTUMIE KWENYE E-mail: kusinileo@gmail.com

Saturday, 25 June 2016

USANGU LOGISTIC YASHAURI MADEREVA KUPIMWA KABLA YA KUPATIWA LESENI



Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Usafirishaji wa Mizigo Usangu Logistic,Ibrahim Ismaili  akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Magari ya kampuni  ya Usafirishaji wa Mizigo Usangu Logistic,yakiwa kazini barabarani

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Usafirishaji wa Mizigo Usangu Logistic,Ibrahim Ismaili  ameitaka serikali kuwapima Madereva wa magari  kabla ya kutoa Leseni ili kuepusha ajali zisizo na lazima na kuliepusha taifa hasara na wimbi kubwa la walemavu wa viungo.
Aliyasema hayo wakati akizungumza na wandishi wa habari ofisini kwake jijini  Dar es Salaam .
Akifafanua zaidi Ibrahimu alisema ajali nyingi nchini zimekuwa zikitokea kwa kusababishwa na uzembe wa madereva  kwani mamlaka husika hutoa leseni lakini hakuna mpango wa kutambua au kumpima muhusika kabla ya kupata leseni
Aidha alisema taifa linaingia hasara kila siku kutokana nan ajali ambazo zingweza kuzuilika kutokana na madereva wengi kutokua na elimu na kutumia kilevi wawapo kazini hali inayohatarisha usalama wao na gari.
 Pia aliwataka Madereva kujenga tabia ya kusoma katika vyuo vinavyotambuliwa na mamlaka husika pia kujali na kuzifata sheria za usalama barabarani kikamilifu
Vile vile alishauri serikali kupunguza Road block (vizuizi) za barabarani kwani wakati wa kusafirisha mizigo kumekuwa na ucheleweshwaji wa barabarani hali inayowapa usumbufu madereva wawapo njiani.
.

No comments:

Post a Comment