Kwa habari zaidi kuhusu ORBIT tembelea tovuti ya: www.orbit-tz.com
KWA MAONI AU USHAURI TUTUMIE KWENYE E-mail: kusinileo@gmail.com

Saturday, 30 May 2015

AHADI ZA LOWASSA KWA WATANZANI





WAZIRI  Mkuu Mstaafu aliyejiuzulu na Mbunge wa sasa wa jimbo la Monduli, Arusha, Edward Ngoyai Lowassa amesema atahakikisha Tanzania inaondokana na msemo wa kuitwa ‘kichwa cha mwendawazimu”.
Lowassa ametamka maneno haya wakati akihutubia kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini Arusha, akitangaza rasmi nia ya kugombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Lowassa  ‘Mzee wa Maamuzi Magumu’ amese iwapo atapitishwa kugombea kitu cha urais na kushinda basi atahakikisha anapambana na udhaifu wa Tanzania katika michezo mbalimbali hadi kufikia kuitwa kichwa cha cha Mwendawazimu.
“Kama nitapata nafasi, basi nitahakikisha Tanzania inaondokana na kuitwa kichwa cha Mwendawazimu,” Amesema Lowassa  na kuongeza: “Tanzania tumekuwa hatufanyi vizuri katika michezo mbalimbali ikiwemo riadha na michezo mingine.”
Lowassa ni kati ya wanachama wa CCM wanaowania nafasi hiyo ya urais kupitia CCM, wengine wanaotajwa ni Benard Membe, Stephen Wasira, Mwigulu Nchemba na wengineo.

No comments:

Post a Comment